0

Mkenya Aliyeorodheshwa Zaidi ya Aliko Dangote Ana Mipango Na Mombasa..... Ni Mipango Gani?

 Aliorodheshwa kua nambari mbili katika orodha ya watu wenye waono makubwa Afrika. Nambari moja alikua Rais wa Tanzania, John Kapombe Magufuli . Katika orodha hio Joe Kariuki aliwapiku vigogo tajika barani kama vile  tajiri mkubwa Africa, Aliko Dangote.
Joe amejulikana sana katika tasnia ya burudani alipokua akimiliki Candy n Candy kabla ya kuanza mradi wa AMSHA MAMA ambao ni mradi wa kuhamasisha akina mama na kuwawezesha kufanya biashara na  kujiendelesha kimaisha.

  1. Wikendi iliyoisha, Joe Kariuki alikua hapa mkoani akiwa ni katika hali ya matayarisho ya tamasha kutambulisha mradi huo hapa mkoani. Joe alitembelea vikundi vya kina mama eneo la Frere town akiwa  pamoja na mkuu wa radio, Pilipili FM, Chris da Bass, mtangazaji wa PiliPili FM Gates Mgenge pamoja na MCA mtarajiwa wa wadi ya Frere, Charles Kitula na aliweza kuwapa wanawake wawili pesa talim kama mtaji wa kuanza biashara ili wweze kujitegemea.
Ziara yake ya hapa mkoani si ndogo kwani ni katika matayarisho ya tamasha kubwa la kutambulisha AMSH MAMA. Uzinduzi huo wa AMSHA MAMA utakua ndio uzinduzi rasmi wa project hiyo inayolenga kuwezesha wanawake 10,000 kufanya biashara na kujitegemea kimaisha. Uzinduzi huo utafanyika katika uwanja wa MAMA NGINA DRIVE, tarehe 30 APRIL na kiingilio kitakua bure,,,wasaanii kama vile TundaMan ambaye ni balozi wa AMSHA MAMA, Tanzania anatarajiwa kuwepo katika uzinduzi huo.
Vilevile, kabla ya tamasha hilo, AMSHA MAMA itakua inatambulishwa Pwani Tarehe 19 April katika sherehe ambao itakhudhuriwa na vikundi takriban 30 kutoka maeneo tofauti hapa Mombasa.

Post a Comment Blogger

Theme images by sebastian-julian. Powered by Blogger.
 
Top