NA.MOHAMED HAMAD MANYARA
CHAMA cha mapinduzi CCM wilayani Kiteto mkoani Manyara kimegawanyika vipande kutokana na joto la kisiasa linaloendelea kupanda kila kukicha kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015
Taarifa za uhakika ndani ya chama hicho zimeeleza kuwa hakuna mahusiano mema ya kikazi kati ya Mjumbe wa Halamshauri Kuu ya CCM Emmanuel Papiani na Mbunge wa Jimbo la Kiteto Benedict Ole Nangoro ambao wote wanawania Jimbo hilo
Akizungumza na MTANZANIA katibu wa Mbunge huyo Singo Ndoera jana alisema Mbunge Nangoro hawezi kuungana na msafara anaofanya Mjumbe wa Halamshauri kuu ya CCM Taifa Emmanuel Papian kwa kuwa unabagua wanachama kwenye msafara wake
“Kiukweli pamoja na kuwa ziara hiyo ni njema kuzungumzia katiba na uandikishaji wa daftari la wapiga kura naweza kusema kuna ubaguzi unaofanywa na uongozi wa msafara huo kwani baadhi ya watu hawatakiwi kuwepo”alisema Ndoera
Alisema ziara aliyomaliza hivi karibuni baada ya hii alimfukuza mwanachama mmoja wa CCM aliyejulikana kwa jina la Dura Msonde katika Kijiji cha Matui kwa madai kuwa Hayupo kwenye kambi yake
Tumeamua kumwachia MNEC amalize ziara yake na kisha nasi tutaanza ya kwetu ambapo nasi tutazunguka wilaya yote kuongea na wananchi ambao wanahamu ya kuongea na Mbunge wao juu ya maendeleo yao
Mjumbe huyo wa CCM Taifa katika ziara yake ameambatana na katibu wa CCM wilaya Abeid Meila, Katibu wa mwenezi Christopher Parmet, na mwenyekiti wa Vijana CCM wilaya Bw,Emmanue na Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Kanal Samweli Nzoka,
Kuhusu tuhuma za kufukuzwa mwanachama huyo kwenye msafara wa MNEC huyo alisema hajamfukuza na wala hana sababu ya kufanya hivyo na kwamba kazi ya chama haina ubaguzi na ndio maana anazunguka na viongozi wa ngazi mbalimbali wa CCM katika kufikisha ujumbe wake
Ujumbe katika ziara hiyo ya MNEC ni kuwataka wananchi kujiandaa kujiandikisha daftari la kudumu la wapiga kura,kusoma katiba pendekezwa na kuipigia kura, na kulaani mauaji yanayoendelea kujitokeza ya wakulima na wafugaji kila mara
Alisema changamoto anayoipata katika ziara yake ni pamoja na kuulizwa maswali mengi kuhusu ahadi alizokwisha kuziahidi wakati wa kumwaombea kura Mbunge huyo zikiwemo za maji,umeme na hata mawasiliano ya simu akisema Mbunge huyo amekuwa mzito kwenda kuongea na wananchi
Mwisho

